Saturday 7 December 2013

BAADA YA KUFUNGIWA MWAKA MMOJA KWA KUTUMIA MADAWA - DECO AKATA RUFAA MAHAKAMANI



Kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea na Barcelona Deco amekata rufaa katika mahakama ya kimataifa ya michezo CAS kupinga adhabu ya kufungiwa mwaka mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madawa yasiyoruhusiwa michezoni.

Deco, 36, ambaye alitangaza kustaafu soka mwezi August mwaka huu, alipimwa na kukutwa na madawa aina ya furosemide mwilini mwake wakati huo akiwa anaichezea klabu ya Brazil - Fluminense mnamo mwezi March.

Kiungo huyo alijitetea kwamba madawa yaliyokutwa mwilini mwake yalitokana na kunywa vinywaji wa vitamin.

No comments: