Sunday 26 January 2014

Dada zetu badiliken hii ni Dunia ya Digital

Siku hizi dada zetu wengi wanamiliki magari. Ujio wa mabenki na utolewaji wa mikopo imewafanya dada zetu wengi kumiliki magari na hivyo kuondokana na usumbufu wa kuparamia daladala.

Lakini kuna tatizo moja ambalo nimeligundua kwa baadhi ya dada zetu wanaomiliki magari, usije ukaona Mdada ameshuka ndani ya gari lake amependeza ukadhani na gari lake ni nadhifu, utakuwa unajidanganya, hebu lisogelee kisha uchungulie ndani utashangaa.

Yaani utakuta gari hilo limegeuka kama nyumba:

Humo humo utakuta kuna containers za kubebea vyakula, na huenda ukakutana na left overs a.k.a kiporo ambacho kinasubiri kupashwa moto kwenye microwave ya ofisini.

Humo humo utakuta Wardrobe yaani ndani ya gari utakutana na pair kadhaa za viatu, mikoba, pair kadhaa za mawani, make ups, mateitei, Magagulo, shumizi na vikorokoro vingine.....

Mimi huwa najiuliza kama hiyo ni nyumba au ni gari.

Msije mkanitia vidole vya macho, naomba mjirekebishe.........

No comments: