Friday 24 January 2014

Mwanamke atekwa na penzi la watoto

MWANAMKE aliyefahamika kwa jina la Bi. Aretas Joseph (48), mkazi wa Kijiji cha Lesoroma, Tarafa ya Usseri, Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, anatuhumiwa kufanya mapenzi na watoto wadogo wa kiume wenye umri kati ya miaka tisa hadi 14.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Robert Boaz, alisema Bi. Joseph alikamatwa Januari 8 mwaka huu, kutokana na ushirikiano uliotolewa na majirani zake.
Alisema vitendo hivyo amekuwa akivifanya muda mrefu ambapo majirani waliweka mtego na kufanikiwa kumkuta chumbani kwake akiwa na watoto watatu wanaume akifanya nao mapenzi.
Aliongeza kuwa, baada ya fumanizi hilo, majirani hao walitoa taarifa polisi ndipo mama huyo alikamatwa na kufikishwa katika Kituo cha Polisi Rombo.
"Hawa watoto baada ya kuhojiwa walisema wapo wanne na siku hiyo mwenzao hakuwepo...walisema huyu mama huwa anawachezea sehemu zao za siri, kuwapaka mafuta na kuwashawishi wafanye mapenzi kwa zamu.
" Uchunguzi wa awali wa polisi unaonesha huyu mwanamke amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana mmoja aliyekuwa amemaliza darasa la saba miaka mitano iliyopita na kujaliwa kuzaa naye mtoto mmoja," alisema .
Hata hivyo, Kamanda Boaz alisema baada ya Idara ya Ustawi wa Jamii kupata taarifa ya uhusiano huo, ilifuatilia na hatimaye kukatisha uhusiano huo

No comments: