Friday 24 January 2014

Rais wa Barcelona ajiuzulu

Sandro Rosell

Rais wa klabu ya Barcelona, Sandro Rosell, amejiuzulu kufuatia madai ya utumizi mbaya wa fedha wakati klabu hiyo ilipomsajili nyota wa Brazil, Neymar mwaka uliopita.

Bwana Rosell, amesema madai yanadhamiria kumharibia sifa na kuwa haya sio ya kweli lakini amehisi hadhi ya heshima ya klabu hiyo itahujumiwa ikiwa ataendelea kuhudumu kama rais wa klabu hiyo.

Mapema wiki hii, gazeto moja nchini Uhispania ilinadi kuwa, klabu hiyo ilitumia Uro milioni arubaini zaidi kuliko ilivyotangazwa kumsajili mchezaji huyo kutoka Brazil.

Ripoti zinasema kuwa babake Neymar na mawakala wengine waliohusika na mkataba huo walilipwa kiasi fulani cha pesa ambacho hakikutangazwa

No comments: