Monday 27 January 2014

SIMBA SC YAANZA MZUNGUKO WA PILI KWA KUWAFUMUA RHINO - MESSI AENDELEZA MAKALI

Ramadhani Singano 'Mess' (kulia), akishangilia bao pekee aliloifungia timu yake katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora katika mchezo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Ramadhani Singano akiipangua ngome ya Rhino Rangers ya Tabora.
Kipa wa Rhino Rangers, Charles Mpinuki akidaka pelnati ya mshmambuliaji wa Simba, ramadhani Singano 'Mess' katika mchezo wa Ligi Kuu.
Beki wa Rhino Rangers, Julius Masunga akitafuta mbinu za kumtoka Haruna Chanongo wa Simba.

Mwamuzi wa pembeni, Frank Komba kutoka Pwani alilalamikiwa na wachezaji wa Simba baada ya kukataa moja ya goli lililofungwa na timu hiyo.

Beki wa timu ya Rhino Rangers, Julius Masunga akiusindikiza mpira wavuni katika harakati za kuokoa, hata hivyo mwamuzi wa mchezo huo alilikataa bao hilo na kulalamikiwa na wachezaji wa Simba, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara kuliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba ilishinda 1-0.

No comments: