Monday 27 January 2014

Uwanja wa Arsenal watia aibu England nzima

ARSENAL Ijumaa iliyopita iliichapa Coventry City na kusonga mbele kwenye Kombe la FA, lakini kali zaidi ilifanywa na mashabiki wao kwenye Uwanja wa Emirates.

Kwenye mchezo huo, baadhi ya taa kwenye majukwaa ya Uwanja wa Emirates zilizima na kuonekana giza jambo lililowafanya mashabiki kuwasha tochi za kwenye simu zao na kupatikana mwanga uliotosha kutambuana na kuendelea kutazama mechi hiyo.

Kilichovutia zaidi, wakati mashabiki wa Arsenal wakiwasha tochi kwenye simu zao ili kupata mwanga, mashabiki wa Coventry City walikuwa wakiimba nyimbo za kuitaka Arsenal kulipa bili ili umeme usiwe unakatika kama ilivyotokea siku hiyo.

Arsenal ilishinda mabao 4-0, shukrani kwa mabao mawili ya Lukas Podolski, Santi Cazorla na Olivier Giroud.

No comments: