Tuesday 18 February 2014

Airtel yazindua mpya ya kisasa zaidi

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imetangaza rasmi huduma ya kisasa ya kifedha kupitia huduma ya Airtel Money.

Huduma hiyo mpya ya kibunifu itatoa uzoefu tofauti wa huduma za fedha kwa wateja wake.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colaso, alisema huduma hiyo ijulikanayo kama ‘Hatoki Mtu Hapa’, itawawezesha wateja wa Airtel kufanya miamala bure bila kikomo kwa kununua kifurushi cha Bure Pack cha wiki au cha mwezi.

“Vifurushi vya Bure Packs vitawapa wateja wa Airtel Money uhuru wa kuchagua kifurushi kinachokidhi mahitaji yao na kuwawezesha kufanya miamala bure bila kikomo kwa wiki au kwa mwezi kulingana na matakwa yao.

No comments: