Tuesday 11 February 2014

Ajali ya ndege yaua 100 Algeria

Ndege ya usafiri ya jeshi imeanguka ikiwa imebeba zaidi ya watu 100.

Redio ya taifa inasema ndege hiyo imeanguka katika eneo la milima katika jimbo la Oum El Bouaghi kusini mashariki mwa mji mkuu , Algiers na ilikuwa imewabeba abiria 103 wakiwemo wafnyakazi wa ndege hiyo.

Kuna taarifa kwamba ndege hiyo ilikuwa imebeba familia za maafisa wa jeshi.

Ndege hiyo ya wanajeshi inaripotiwa kuanguka katika eneo lililo na milima mingi mashariki ya nchi hiyo. Kituo cha Redio ya nchi ya Algeria inasema kuwa kulikuwa na waabiri 103, wakiwemo watumishi wa ndege hiyo.

Hakuna ripoti rasmi za majeruhi, ila vituo vya habari vya nchi hiyo vinapeana matumaini kwa uchache mno juu ya manusura.

Ndege hiyo inasemekana ilikuwa ikibeba wanajeshi na watu wa familia zao waliokuwa wakisafiri kuelekea jiji la Constatine. Jeshi halijatoa taarifa yoyote mpaka sasa.

No comments: