Wednesday 12 February 2014

Katibu mkuu wa UN aonya kuhusu ghasia-CAR

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon ameonya kuwa ghasia zinazoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, zinaweza kuligawa taifa hilo na kuwatenga kabisa Wakristo na Waislamu.

Bwana Ban ki ameiomba Ufaransa kuwatuma wanajeshi zaidi wa kutunza amani katika taifa hilo, ambalo limekumbwa na mapigano ya kidini tangu mapinduzi ya kijeshi Machi mwaka uliopita.

Katika siku za hivi karibuni, maelfu ya Waislamu wamekimbilia nchi jirani, ili kuepuka mapigano hayo.

Katika ripoti mpya iliyochapishwa na shirika la kutetea haki za kibinadam, la Amnesty International, inasema kuwa wanajeshi wa Kimataifa wa kutunza amani nchini humo wameshindwa kuzuia kile ilichokitaja kama mapigano ya kidini yanayodhamiria kuwaangamiza raia wote ambao ni Waislamu.

Katika ripoti yake shirika hilo linasema kuwa vikosi vya kimataifa vimesita sita kukabiliana na wanamgambo wa AntiBalaka ambao wengi wao ni Wakristo wanaoendesha mashambulizi dhidi ya Waislam.

Jamii nyingi za raia wanaoishi katika miji ya Kaskazini Magharibi mwa taifa hilo wameachwa bila ulinzi.

No comments: