Tuesday 11 February 2014

Keshi awachagua wachezaji wapya

Kocha wa Nigeria Stephen Keshi, amewajumuisha wachezaji watatu ambao hawajawahi kuichezea timu ya taifa ya nchi hiyo Super Eagles, katika kikosi chake kitakachochuana na Mexico, mjini Georgia, Atlanta tarehe tano mwezi ujao, katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.

Wachezaji hao ni pamoja na Imoh Ezekiel, Ramon Azeez na Michael Uchebo

Mshambulizi matata wa Standard Liege Imoh Ezekiel, sasa amepewa fursa ya kujitafutia nafasi katika kikosi cha Nigeria, kitakacho wakilisha taifa hilo kwenye fainali ya kombe la dunia nchini Brazil.

Msimu huu Ezekiel, mwenye umri wa miaka 20, amefunga magoli tisa na kwa muda mmrefu amekuwa katika hali nzuri hali iliyomfanya kocha Keshi kumjumuisha kwenye kikosi chake.

Uchebo, ambaye anasakata soka nchini Ubelgiji, ameifunguia klabu klabu yake ya Cercle Brugge amegoli matano naye mcheza kiungo Azeez kwa upande wake hajakuwa na bahati ila amekuwa miongoni mwa wachezaji ambao wanauwezo wa kucheza safu ya kati na ushambulizi kwa wakati mmoja.

Wachezaji wawili wa kutegemewa wa Nigeria, Shola Ameobi wa NewCastle na Brown Ideye wa Dynamo Kiev kwa sasa wako chini kimchezo na aliyekuwa mshambulizi wa timu ya taifa ya Nigeria Uchebo huenda akajikatia tikiti ya kwenda Brazil.

No comments: