Tuesday 18 February 2014

Leonel Messi avunja record

Lionel Messi anaweza kuvunja rekodi yoyote iliyokuwa kichwani mwake,” kwa mujibu wa kocha Barcelona, Gerardo Martino baada ya kumshuhudia nyota wa Argentina akiwa mchezaji watatu kwa wachezaji waliofunga mabao mengi La Liga.

Messi alifunga mabao mawili wakati Barca iliposhinda 6-0 dhidi ya Rayo Vallecano na kumfunika mshambuliaji wa zamani Real Madrid, Raul aliyefunga mabao 228 katika La Liga.

“Amepoteza kumbukumbu ya rekodi zake alizovunja,” Martino aliimbia Barcelona.

Messi amefunga mabao 228 La Liga ikiwa ni mechi yake ya 263, akifunika rekodi ya gwiji wa Real Madrid, Alfredo Di Stefano aliyefunga mabao 227 katika mechi 359, na sasa anazisaka rekodi za Telmo Zarra (251) na Hugo Sanchez (234).

Kwa sasa amebakiza mabao sita tu kuifikia rekodi ya Raul ya kufunga mabao 71 katika Ligi ya Mabingwa.

No comments: