Monday 24 February 2014

simba ya pigishwa guu pande guu sawa na wanajeshi



Simba yapigishwa kwata na maafande wa JKT Ruvu
Monday, February 24 2014, 8 : 41

TIMU ya Simba jana ilikiona cha mtema kuni baada ya kuzabwa mabao 3-2 na timu ya maafande JKT Ruvu katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Bao la kwanza la JKT Ruvu lilipatikana katika dakika ya 13 lililofungwa na Hussein Bunu baada ya mabeki wa Simba kujichanganya.
Dakika ya 18 nusura Amis Tambwe aipatie bao Simba baada ya kuachia shuti kali lililopaa juu ya lango JKT Ruvu.
Timu ya Simba ilifanya mabadiliko dakika ya 22 kwa kumtoa Said Ndemna na nafasi yake kuchukuliwa na Ali Badru kwa ajili ya kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji.
JKT Ruvu iliandika bao lake la pili katika dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza lililofungwa na Emmanuel Swita kwa mkwaju wa penalti iliyosababishwa na Henry Joseph baada ya kumfanyia madhambi mchezaji wa JKT Ruvu katika eneo la hatari.
Kipindi cha pili JKT iliingia kwa nguvu na kufanikiwa kupata bao la tatu kupitia kwa Bunu tena baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Damas Makwaya, dakika ya 57 nusra Amis Tambwe aipatie Simba bao.
Dakika ya 71 Simba ilifanya mabadiliko tena kwa kumtoa nje Badru na nafasi yake kuchukuliwa na Issa Rashid 'Baba Ubaya', Awadh Juma aliikosesha Simba bao la wazi akiwa ndani ya 18 akiwa yeye na mlinda mlango, lakini alishindwa kufunga.
Simba ilipata bao la kwanza katika dakika ya 63 ya mchezo kwa mkwaju wa penalti uliokwamishwa wavuni na Tambwe baada ya Amri Kiemba kuchezewa rafu katika eneo hatari.
Dakika ya 82 Simba ilipata bao kupitia kwa mchezaji Amis Tambwe baada ya kupoke pasi safi kutoka kwa Uhuru Selemani.
Wakati huo huo, mchezo kati ya Azam FC na Prison ya Mbeya ulimalizika kwa suluhu kwa kufungana mabao 2-2 huku kila timu ikionesha kandanda safi ya kuvutia.

No comments: