Friday 28 March 2014

Babu Etoo aipa adhabu Man U

Samuel Eto'o akishangilia baada ya kufunga goli.
LONDON, ENGLAND

MANCHESTER United basi tena. Ndicho unachoweza kusema baada ya mabingwa hao wa Ligi Kuu England kugeuzwa vibonde kwenye ligi hiyo kufuatia kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Chelsea jana Jumapili kwenye Uwanja wa Stamford Bridge.

Samwel Eto’o alifunga ‘Hat-Trick’ kuifanya Chelsea kuzidi kuweka hai matumaini yao ya kushindania ubingwa wa ligi hiyo msimu huu baada ya kufikisha pointi 49, pointi mbili nyuma ya vinara Arsenal.

Eto’o alifunga katika 17, 45 na 49. Manchester United iliyomaliza ikiwa pungufu kufuatia kadi nyekundu ya Nemanja Vidic ilipata bao lake kupitia kwa Javier Hernandez kwenye dakika 78.

Mchezo mwingine wa ligi hiyo, Tottenham Hotspur waliichapa Swansea City mabao 3-1, shukrani kwa mabao mawili ya straika Emmanuel Adebayor na moja la kujifunga la Chico. Bao la Swansea lilifungwa na Wilfried Bony.

No comments: