Friday 28 March 2014

Barca na Uhispania kumkosa Valdez

Mlinda mlango wa Barcelona na timu ya taifa ya uhispania, Victor Valdes hatashiriki fainali za Kombe la dunia baada ya kupata jeraha kwenye mshipa wa mguu.

Victor mwenye umri wa miaka 32 aliondolewa uwanjani kwa machela wakati wa mechi kati ya Barcelona na Celta Vigo, ambapo Barcelona iliinyuka timu hiyo magoli 3-0 siku ya jumatano.
Kipa wa Barcelona Victor Valdez ajeruhiwa

Klabu ya Barcelona imethibitisha kuwa mchezaji huyo amepata jeraha na kuwa atahitaji kufanyiwa upasuaji.

Inaelezwa kuwa kutokana na hali hii huenda Valdes ukawa ndio mchezo wake wa mwisho akiwa na Barcelona na ataondoka kwenye klabu hiyo mkataba wake utakapomalizika kipindi cha majira ya joto.

Kocha wa Barcelona, Gerardo Martino amesema hakuna mpango wa kumtafuta mlinda mlango mwingine na kuwa atamaliza msimu huu na kikosi alichonacho.

Victor alipata jeraha dakika ya 22 katika dimba hilo lililokuwa Nou Camp, muda mfupi baada ya kupangua mpira wa adhabu wa Celta Vigo.

Valdes, ambaye ambaye ameichezea Barcelona kwa miaka 12, alikuwa akitegemewa kupambana na Iker Casillas kupata nafasi ya kuidakia timu ya taifa ya Uhispania katika michuano ya kombe la dunia

nchini Brazil mwaka huu lakini fursa hiyo imeonekana kuwa finyu kwake.

Valdes amepata jeraha ikiwa ni mara ya pili katika msimu huu mara ya kwanza alipata jeraha kwenye kifundo cha mguu wakati Uhispania ilipocheza mechi ya kirafiki na Afrika kusini mwezi Novemba

mwaka jana na kufungwa 1-0.

Jeraha hilo lilimfanya Valdes kukosa mechi nane ya Barcelona.

No comments: