Friday 14 March 2014

Coastal kuifuata Azam

TIMU ya Coastal Union, yenye maskani yake jijini Tanga, inajiandaa vizuri kukabiliana na joto katika mchezo wao dhidi ya Azam utakaopigwa Jumamosi ya Machi 15, katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Mechi hiyo inachezwa huku kukiwa na marekebisho kadhaa, hasa kati ya Simba na Costal, waliopangwa kucheza Jumatano, kabla ya mechi hiyo kusogezwa mbele hadi Machi 23.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Costal Union, Hafidh Kido, alisema kuwa wanajiandaa vyema ili kusaka ushindi dhidi ya Azam.

Alisema ingawa wamepata matokeo mabaya ya sare dhidi ya Ashanti United, ila bado hawajakata tamaa katika patashika ya Ligi ya Tanzania Bara.

“Coastal bado hatujakatishwa tamaa katika harakati za kuiweka juu zaidi timu yetu, hivyo kwa sasa tunajiandaa kuwakabiri Azam.

“Naamini utakuwa ni mchezo mgumu kupita kiasi, ukizingatia kuwa Azam wao wanasaka ubingwa, hivyo watataka mbeleko kutoka kwetu, jambo ambalo haliwezekani kirahisi,” alisema.

Simba inayonolewa na kocha wake Zdravko Logarusic, imeshindwa kuonyesha cheche za kuunyaka ubingwa wa Tanzania Bara, baada ya kuendelea kupata matokeo mabaya katika mechi zake.

No comments: