Friday 28 March 2014

Kura ya maoni kuhusu Crimea inautata

Baraza la umoja wa mataifa limetangaza matokeo ya azimio ambalo limeharamisha hatua ya Urusi kuandaa kura ya maoni kuhusu eneo la Crimea na kuunga mkono uhuru wa Ukraine.
Umoja wa mataifa unaunga mkono uhuru wa Ukraine

Nchi 100 zimepiga kura kuunga mkono Azimio hilo huku nchi 11 zikipinga.

Azimio hilo lililowasilishwa mbele ya baraza la Umoja wa Mataifa na Ukraine linanuia kuisisitizia Urusi kwamba inakabiliwa na tishio la kuendelea kutengwa zaidi kidiplomasia na jamii ya kimataifa.

Limehimiza haki ya taifa la Ukraine na kuitaja kura ya maoni iliyofanyika Crimea hivi karibuni kama isiyohalali.

Akizungumza baada ya azimio hilo kupitishwa,balozi wa Muungano wa Ulaya katika umoja wa mataifa , Thomas Mayr-Harting, amesema sio haki kutumia nguvu kubadili mipaka ya nchi.

Naye waziri wa mambo ya nje wa Ukraine , Andriy Deshchytsia, ameelezelea kudhirishwa na azimio hilo la Umoja wa Mataifa.

Akizungumza kabla ya azimio hilo kupitishwa balozi wa Urusi katika Umoja wa mataifa Vitaly Churkin aliomba baraza la Umoja wa mataifa kuheshimu matokeo ya kura ya maoni iliyofanyika Crimea ambapo raia wengi walipendelea kujiunga na Urusi.

Ukraine inatarajia kuwa kupitishwa kwa azimio hilo kutaipa shinikizo zaidi Urusi na kuionya dhidi ya kuendelea kuvamia maeneo yake.

No comments: