Friday 14 March 2014

MB; DOG kuachia song Mpya hivi karibuni

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Mbwana Mohammed maarufu kama Mb Dogg, yupo kwenye mipango ya kuachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Baby mbona umenuna?
Mb Dogg pichani, wimbo wake mpya wa 'Baby Mbona Umenuna' utakuwa balaa na unatarajiwa kumuweka tena kileleni.


Wimbo huo umerekodiwa katika Studio za Maccopa, ambapo unatarajiwa kurudisha makali na heshima ya msanii huyo aliyewahi kuwika katika tasnia hiyo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Qs Mhonda J Entertainment, Joseph Mhonda, alisema kwamba wimbo huo ni moto wa kuotea mbali ambao kwa kiasi kikubwa utamuweka juu zaidi.


Alisema kwamba Mb Dogg ni msanii aliyejichimbia kwa muda mrefu akiwa na mahitaji ya kurudi kwenye nafasi zake za juu alipokuwa awali.


“Sisi kama Kampuni tunaofanya kazi na Mb Dogg tunaamini kabisa huu ni wakati wake wa kurudi tena kileleni ili aendeleze makali yake ya awali.

“Baby Mbona umenuna ni wimbo ambao kwa hakika utadhihirisha ubora wa mwimbaji huyu wa Latifa na nyinginezo zilizomuweka kileleni,” alisema.

Mb Dogg anatokea katika kampuni hiyo kwa sasa, akiwa sambamba na Nay wa Mitego anayetamba na wimbo wa Muziki Gani, aliyeimba na Diamond.

No comments: