Sunday 13 April 2014

Boko Haram imeshaua watu zaidi ya laki moja

Imebainika kuwa wanamgambo wa kiislamu kazkazini mwa Nigeria wamewaua zaidi ya watu laki moja na arubaini na tano katika misururu ya mashambulizi juma lililopita.

Sineta wa jimbo la kazkazini mashariki la Borno Ahmed Zannah ameiambia BBC kwamba mauaji hayo yalifanyika katika maeneo matatu tofauti yaliopo mashambani.

Amesema kuwa taassi moja ya kutoa mafunzo ya elimu ndio iliokuwa ya kwanza kulengwa ambapo wanamgambo hao waliwaua walimu watano kabla ya kuwatekanyara wake zao kadhaa.

Wapiganaji hao wanaoshukiwa kutoka katika kundi la wanamgambo wa Boko haram baadaye walivamia vijiji viwili katika eneo la mashambani karibu na mpaka na Cameroon.

No comments: