Sunday 13 April 2014

Guinea Bissau kufanya uchaguzi kumchagua rais wao

Uchaguzi wa urais na maeneo bunge unafanyika katika taifa dogo la afrika magharibi Guinea Bissau.

Ni uchaguzi wa Kwanza tangu kufanyika kwa mapinduzi miaka miwili iliopita -ikiwa ni hatua ya hivi karibuni ya kijeshi ambayo imesaidia kuhakikisha kwamba hakuna raisi aliyechaguliwa ambaye amefanikiwa kuiongoza Guinea Bissau kwa kipindi chote alichochaguliwa tangu taifa hilo lijipatie Uhuru wake kutoka kwa Ureno mnamo mwaka 1974.

Kiongozi wa mapinduzi hayo Antonio Indjai aliikabidhi mamlaka serikali ya raia mnamo mwaka 2012 iliopewa wajibu wa kuandaa Uchaguzi huo.

Indjai alifunguliwa mashtaka nchini marekani kwa madai ya kufanya biashara ya mihadarati pamoja na kuwauzia silaha waasi wa Colombia.Wagombea 13 wanawania wadhfa wa urais.

Iwapo mmoja wao hatashinda kwa wingi wa kura basi uchaguzi huo utaenda kwa awamu ya pili mnamo mwezi May.

No comments: