Tuesday 29 April 2014

Kimbunga cha Mississippi


Nchini Marekani Kimbunga kimepiga jimbo la Mississippi
kimbunga-cha-mississippi
Baada ya kupiga majimbo ya Arkansas na Oklahoma, kimbunga kimepiga jimbo la Mississippi.
Katika mji wa Tupelo iliyoko Kaskazini mwa jimbo hilo kimbunga kilipiga na kukata nyaya za stima, kungoa miti na kusababisha uharibifu wa nyumba.
Maafisa wahusika pamoja na wale wakujitolea walitoa msaada kwa walioathiriwa na kimbunga hicho.
Wataalam wametoa tahadhari kwa wakaazi wa majimbo ya kati na kusini kuwa huenda kimbunga kikapiga tena kutokana na mabadiliko katika hali ya anga.
Watu 17 walifariki katika majimbo ya Arkansas, oklahoma na Iowa kutokana na Vimbunga.

No comments: