Monday 28 April 2014

Serikali mpya imeingia mamlakani nchini Serbia.

serikali-mpya-nchini-serbia
Bunge la Serbia limepitisha serikali yenye mawaziri 16 iliyochaguliwa na mkuu wa chama cha "Serbian Progressive Party" (SNS) Aleksandar Vuçiç.
Wabunge 198 kati ya wabunge 228 waliokuwepo bungeni walipiga kura kukubali orodha iliyowasilishwa bungeni.
Katika hafla ya kuapishwa iliyohudhuriwa na Rais wa jamhuri ya Serbia, Waziri mkuu Vuçiç alisema kuwa wataongoza nchi hiyo kwa njia ya uadilifu.
Serikali hiyo mpya itawajumuisha Ivitsa Daçiç mkuu wa chama cha "Serbian Socialist Party" (SPS) ambaye atachukua wadhfa wa waziri wa mambo ya nje na Rasim Lyayiç ambaye ni mkuu wa chama cha "social Democratic Party" (SDPS) atakayechukua wadhfa wa waziri wa Biashara, Mawasiliano na Utalii. Waziri Rasim Lyayiç aliwahi kuhudumu katika wizara hii hapo awali.
Chama cha "Serbian Progressive Party" (SNS) kinachoongozwa na Aleksandar Vuçiç kilitwaa ushindi katika uchaguzi wa mapema uliofanyika tarehe 17 mwezi Machi nchini Serbia.

No comments: