Tuesday 13 May 2014

Daktari adai mwanariadhaPistorius afanyiwe uchunguzi wa kiakili


Daktari amesema Pistorius hapaswi kumiliki Bunduki hasa kutokana na matatizo yake ya kiakili
Upande wa mashitaka katika kesi dhidi ya mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius umetoa ombi la kutaka mwanariadha huyo kufanyiwa uchunguzi wa kiakili wakati kesi hiyo ikiendelea.
Wakili Gerrie Nel aliwasilisha ombio hilo kwa mahakama baada ya mtaalamu wa matibabu ya kiakili Merryll Vorster kusema kuwa Pistorius ni hatari kwa jamii.
Awali daktari Vorster alisema kwamba mkimbiaji huyo anakumbwa tatizo la kupatwa na wasiwasi wakati wote tangu utotoni mwake na kwamba ni muoga wa vitendo vya uhalifu.
Pistorius amekana madai ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp mwaka jana. Alisema kuwa alimpiga risasi kwa bahati mbaya akidhani kuwa alikuwa jambzi aliyekuwa amevamia nyumba yake.
Upande wa mashitaka unatuhumu upande wa utetezi kwa kubadilisha kauli yake mwanzo kwa kusema kuwa Pistorius alilamizimika kufyatua risasi baada ya kuhofia usalama wake na sasa anasema kuwa alikuwa na tatizo la kiakili.
Bwana Nel alisema kwamba uchunguzi huo ni muhimu hasa kwa sababu ya kuhakikisha kuwa haki inatendeka kwa hivyo ni sawa kwa Pistorius kwenda kuchunguzwa.
Daktari, Vorster aliambia mahakama kwamba hasemi kuwa Pistorius ana tatizo la kiakili na kwamba bado anaweza kutenda vyema kazi yake ya riadha na pia bado ana uwezo wa kuwasiliana na watu wengine vyema tu.
Lakini alisema kuwa watu wenye tatizo la kuwa na wasiwasi wakati wote kama Pistorius hawapaswi kuruhusiwa kujihami.

No comments: