Tuesday 13 May 2014

Kanda ya Jay-Z akichapwa yazua hasira

Jay-Z na mkewe wa mika sita Beyonce Knowles
Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia kanda ya video iliyozuka ikionyesha dadake mwanamuziki wa kimataifa Beyonce Knowles , Solange Knowles akimchapa makonde mwanamuziki Jay-Z ambaye pia ni shemeji yake katika lifti.
Wakuu wa hoteli ambako kisa hicho kinadaiwa kutokea mjini New York, 'The Standard Hotel' wamesema kuwa wanachunguza ambavyo kanda ya kisa kilichotokea ndani ya Lifti iliweza kusambazwa baada ya kanda hiyo ya video kuzuka katika mtandao mmoja wa udaku TMZ.
Hata hivyo kanda hiyo haikuwa na sauti bali ilionyesha tu kitendo cha dadake Beyonce akimpacha Jay-Z na hata kujaribu kumpiga teke mara mbili wakiwa ndani ya lifti hiyo pamoja na Beyonce na mlinzi mmoja wa Jay-Z aliyejaribu kumzuia Solange.
Kanda hiyo ilizuka baada ya Beyonce aliyekuwa ameambatana na Jay Z ambaye ni mumewe wa miaka sita pamoja na Solange kuhudhuria tamasha la kifahari mjini New York tarehe tano Mei.
Dadake Beyonce Solange Knowles
Mlinzi wa Jay-Z anaonekana katika kanda hiyo akijaribu kumzuia Solange mwenye umri wa miaka 27 aliyeonekana kuwa na hasira mno kutomchapa Jay-Z amwenye umri wa miaka 44 akiwa amesimama kando ya mkewe wa miaka sita Beyonce.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, taarifa kutoka kwa maafisa wa hoteli ambamo kisanga hicho kilitokea walielezea kukasirishwa na mtu ambaye aliisambaza kanda hiyo kwenye internet na hata kutishia kumchukulia hatua pindi atakapojulikana.
"tumeshtushwa sana na kukasirishwa na mtu aliyekiuka sheria zetu za faragha ambazo wageni wetu wanathamini sana, '' ilisema taarifa kutoka kwa wakuu wa hoteli hiyo.
"tunachunguza hali hiyo na pia yeyote atakayepatikana na hatia ataadhibiwa vikali.''
Wasimamizi wa Beyonce walikataa kuzungumzia kisa hicho.

No comments: