Thursday 22 May 2014

Mapigano bado yanaendelea Libya

mapigano-yanaendelea-katika-mji-mkuu-wa-libyaKundi la waasi lilishambulia jengo la kikosi cha wanaanga kwa kutumia ndege.

Kundi la waasi lilishambulia jengo la kikosi cha wanaanga kwa kutumia ndege.
Ilibainishwa kuwa katika mapigano hayo yasadikiwa wapiganaji wawili raia wa Mali waliuawa.
Aidha kamanda wa kikosi cha majini alinusurika kuuawa na kujeruhiwa kidogo mjini Tripoli.
Mjini Binghazi nako mkandarasi mmoja raia wa China aliuawa.
Kwa upande mwingine, wizara ya mambo ya ndani ilikanusha madai kwamba jeshi linamuunga mkono Brigedia Generali mstaaf Halifa Haftar katika mapambano.
Msimamizi wa mambo wa kigeni katika wizara ya mambo ya ndani, Salih Mazik alieza katika taarifa wakati wa mahojiano na agenti maalum wa habari LANA katika televisheni kwamba  wizara inayayaunga mkono majeshi yanayoongozwa na Haftar.
Mazik, "sio kwa ajili ya Haftar, tupo kwa ajili ya wananchi wa Libya". Alisema.
LANA ilibainisha kuwa kulingana na afisa  wa wizara alivoeleza katika habari, wizara ya mambo ya ndani "imechagua mapenzi ya watu na kwamba ni heshima kupambana na ugaidi.
Wakati huohuo Umoja wa Warabu umeamua kukutana kujadili mgogoro wa Libya.

No comments: