Sunday 8 June 2014

DRC yawasihi waasi kusalimisha silaha haraka iwezekanavyo

DRC yasisitiza kupokonywa silaha waasi wa RwandaSerikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesisitiza kupokonywa silaha waasi wote wa Rwanda walioko nchini humo. Lambert Mende Omalanga, Waziri wa Habari na msemaji wa serikali ya Kongo amesema leo kuwa, serikali ya Kinshasa ipo tayari kuwapa fursa nyingine waasi wa Rwanda wa FDLR ili waweke silaha zao chini. Omalanga ameongeza kuwa, iwapo waasi hao hawatajisalimisha wenyewe katika muda utakaopangwa, serikali ya Kongo itafanya operesheni ya kuwapokonya silaha kwa nguvu. Waasi 100 wa Kihutu Mei 30 walijisalimisha na kukabidhi silaha zao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Licha ya kusambaratishwa kundi la waasi wa M23 lililokuwa likihesabiwa kuwa muhimu zaidi nchini humo, lakini bado amani na utulivu haujaimarishwa kikamilifu nchini Kongo kutokana na kuwepo makundi mengine ya waasi na ya upinzani. 

No comments: