Monday 2 June 2014

Mama zitto afariki

Mama Zitto Kabwe afarikiBUNGE Maalum la Katiba limepata pigo baada ya kuondokewa na mjumbe wake, Shida Salum (64), ambaye ameugua kwa muda mrefu.
Shida ambaye pia ni mama mzazi wa mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema), amesumbuliwa na maradhi ya saratani ya shingo ya kizazi na hivyo kushiriki vikao vya awali pekee vya utungwaji wa kanuni za Bunge hilo.
Kwa mujibu wa Zitto, mama yake ambaye alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Taifa na Mwenyekiti wa Watu wenye Ulemavu nchini, alikumbwa na mauti saa tano asubuhi jana hospitalini hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari, muda mfupi kabla ya sala ya kuombea maiti katika Msikiti wa Maamur ulioko Upanga, Zitto alisema mama yake alizaliwa Julai 1950 na kusoma shule ya sekondari Tabora.
Kwa mujibu wa mbunge huyo, mama yake alikuwa akisumbuliwa na saratani ya shingo ya kizazi ambapo amepata matibabu katika hospitali za ndani na nje.
Shida ambaye pia alikuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, ameacha watoto 10 ambapo sita ni wakiume na wanne ni wa kike.
Akizungumzia taratibu za kibunge, Katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashilila alisema kifo cha mtu ambaye si mbunge taratibu za mazishi hushughulikiwa na familia.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano), Steven Wassira alisema Shida alikuwa mwanasiasa anayelipenda taifa lake.
Mwili huo ulisafirishwa jana kwenda mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi yatakayofanyia leo eno la Mwanga.

No comments: