Saturday 25 October 2014

kiwanda cha Mount Meru Oil Millers singida chaungua Moto

Kiwanda kikubwa cha usindikaji mafuta ya alizeti katika Afrika Mashariki kilichoko , mkoani SINGIDA kinaungua moto jana ambao mpaka sasa umeteketeza maghala zaidi ya matano yanayotumika kuhifadhi mafuta ghafi pamoja na mashudu ya alizeti.

Moto huo ulianza majira ya saa tano za usiku ambapo mpaka mchana huu(jana) jitihada za kuzima moto huo kwa kutumia magari ya zimamoto toka SINGIDA na Mkoa wa MANYARA zinaendelea .

Chanzo cha moto huo inasadikiwa kuwa ni mashudu yaliyokuwa yamehifadhiwa katika ghala mojawapo la kiwanda hicho, cha MOUNT MERU OIL MILL.

Mkuu wa wilaya ya SINGIDA mjini QUEEN MLOZI ambaye alikuwepo katika tukio hilo ameeleza jitihada zilizofanyika kuhakikisha kuwa moto huo unadhibitiwa.

Hasara iliyoopatikana mpaka sasa haijweza kufahamika mara moja mpaka hapo tathimini halisi itakapofanyika.

No comments: