Tuesday 21 October 2014

Kutupwa segerea kwa halima mdee kwa zua Makubwa

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee ameelezea mambo matano aliyokutana nayo katika gereza la Segerea Dar es Salaam alipokaa mahabusu kwa saa 24 kwa tuhuma za kuongoza maandamano yasiyokuwa na kibali Oktoba 4 mwaka huu jijini humo.
Akizungumza jana jijini hapa alisema,akiwa humo alikutana na wasichana wadogo ambao walimweleza wamefika hapo kutokana na kudai haki zao, lakini kwa kuwa wamekosa watetezi wamejikuta wakisota gerezani
Aliongeza: “Mpango wa kupunguza wafungwa wenye vifungo vifupi vifupi unaonekana kukwama, gereza haliendani na wingi wa watu waliomo.
“Kuna wasichana wadogo wengi sana, wanaochukuliwa mikoani kuja kufanya kazi za ndani, wakifika huku wanafanya kazi hizo lakini mwajili wake anaposhindwa kuwalipa na binti huyu akianza kudai haki yake mwajiri anambabikia kesi.
Mdee ambaye pia ni Katibu wa Kanda ya Mashariki wa Chadema alisema kesi za mauaji na wizi zimekuwa zikichelewa, jambo linalowakatisha tamaa washitakiwa kutokana na kukaa muda mrefu.
“Unakuta mtu kweli anajulikana kaua au mwingine kaiba, lakini upelelezi wake utachukua miaka mingi ni rai yangu kwamba umefika wakati uwepo utaratibu wa kupunguza mrundikano’ alisema .
Mdee alisema licha ya gereza kuwa sehemu ya kurekebisha tabia za watu, lakini hali kama hiyo imegeuka kuwa eneo la kufundishia mbinu chafu za kibiashara..
Wasichana wadogo wanafundishwa biashara chafu na waliowazidi umri,wakitoka wanakuwa wamoja na kuanzisha makundi ya uchangudoa” alisema.
Mbunge huyo alisema Serikali ina kazi kubwa ya kukomesha vitendo hivyo na kwamba alipokuwa mahabusu alijifunza mambo mengi.
“Nilipofikishwa kule ilikuwa imeshafika saa 11 jioni, nililetewa ugali ambao haukuwa umeiva, mchicha wenyewe umekomaa na kama ni dagaa basi hawaoshwi wakitolewa katika gunia tu, wanapikwa hivyo hivyo na michanga. Uji ndiyo usiseme sasa fedha za bajeti huwa zinakwenda wapi kama hali ndiyo hiyo,” alihoji Mdee
Mdee alisema licha ya gereza kuwa sehemu ya kurekebisha tabia za watu, lakini kwa hali kama hiyo imegeuka kuwa eneo la kufundishia mbinu chafu za kibiashara.
“Hawa dada zetu wadogo wanaowekwa huko, wanakutana na mi dada iliyokubuhu mitaani kwa vitendo vya kuendesha biashara ya ngono, ikikutana na hao inawafundisha hao wasichana mbinu chafu.”

“Unakuta inawaeleza kwamba unajua kule mtaani kuna biashara ambayo ina lipa kuliko hiyo ya kazi za ndani, hivyo mkitoka tutakwenda kuwafundisha ni kweli wakitoka wanakuwa timu moja wanaanzisha makundi ya machangudoa,” alisema Mdee
Aliongeza: “Serikali ina kazi kubwa ambayo inatakiwa kuifanya kukomesha vitendo hivi, lakini nimefurahi nimewekwa ndani kwani nimeweza kujifunza kitu nikiwa humo na ninatamani siku moja nirudi tena ingawa walinitoa mapema ili nisijue siri za humo zaidi.”

No comments: