Monday 20 October 2014

Manyika JR aibuka kuwa mchezaji bora wa wiki kwa mujibu wa GOAL.COM

Goal Player of the week: Manyika PeterKipa huyo licha ya udogo wake wa umri kwa kucheza pambano kubwa kama hilo alionyesha kutokuwa na wasiwasi na aliwakatisha tamaa mashabiki wa Yanga kwa kudaka krosi zote
KIPA chipukizi wa Simba Manyika Peter ,ameibuka kuwa mchezaji bora  wa wiki baada ya kuonesha kiwango kizuri katika mechi iliyowakutanisha wapinzani wa jadi Simba na Yanga iliyochezwa Jumamosi kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam.
Manyika ameingia kwenye historia ya kuwahi kucheza mechi ngumu ya watani wa jadi akiwa ni mchezaji mwenye umri mdogo zaidi na kufanya vizuri kwa kumaliza dakika zote 90 bila kufungwa na washambuliaji wa Yanga Geilson Santos JAJA,Hamisi Kiiza na Andrey Coutinho.
Kipa huyo licha ya udogo wake wa umri kwa kucheza pambano kubwa kama hilo alionyesha kutokuwa na wasiwasi na aliwakatisha tamaa mashabiki wa Yanga kwa kudaka krosi zote pamoja na kona zilizokuwa zinaelekezwa kwenye lango lake.
Katika muda wote wa dakika 90 Manyika Peter,alionekana kutulia na kuwapanga vyema mabeki wake nahodha Joseph Owino na Hassani Isihaka na kupangua kwa umahiri mkubwa mashuti ambayo yalikuwa yakielekezwa langoni mwake.
Pambano hilo ndilo lililokuwa la kwanza kwa kipa chaguo la tatu kuidakia Simba tangu aliposajiliwa msimu huu na hiyo ilitokana baada ya makipa Ivo Mapunda na Hussien Sharifu kuumia siku chache kabla ya mpambano huo wa watani wa jadi.

No comments: