Sunday 9 November 2014

Mtibwa baba lao, mbeya city yawa kibonde

http://www.kabumbu.co.tz/wp-content/uploads/2014/09/mbeya-city.jpg
Waliofulia msimu huu, Mbeya City
WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikienda mapumziko, Mtibwa Sugar imethibitisha kuwa ndiyo timu bora mpaka sasa ikiwa kileleni mwa msimamo na pointi zake 15 baada ya mechi saba, kadhalika ikiruhusu mabao matatu tu huku timu nyingine 'urojo' kwa kuwa na kuta laini ziliruhusu magoli mengi.
Mtibwa inayonolea na kocha kijana mzawa, Mecky Mexime imezishinda hata timu kubwa zilizotamba kabla ligi haijaanza kwa usajili wa mamilioni ya fedha, huku washambuliaji wake wawili, Ame Ally Zungu na Ali Shomari wakifunga jumla ya mabao saba kuonyesha kombinesheni yao ilivyokuwa kali zaidi.
Magoli mengine ya Mtibwa yamefungwa na wakongwe Mussa hassan Mgosi mwenye mawili na Vincent Barnabas.
Mbeya City iliyosumbua msimu uliopita ikiicheza ligi hiyo kwa mara ya kwanza imejikita ndiyo nyonge zaidi msimu huu kwa kuburuza mkia ikiwa na pointi tano tu baada ya mechi saba ilizocheza kitu kilichowaacha mashabiki wa soka wa klabu hiyo kushindwa kuamini hali iliyowakuta.
Timu hiyo inayofundishwa na Juma Mwambusi Kocha Bora msimu uliopita imeshinda mara moja tu na kupoteza mechi nne na kuambulia sare michezo mitatu.
Ndanda iliyokuwa ikipewa nafasi kubwa ya kutamba na Mbeya City wenyewe nao wameoonekana siyo lolote baada ya kushika nafasi ya pili toka mkiani ikiwa na pointi sita tu iliyotoakana na kushinda mechi mbili na nyingine zilizosalia imepoteza ikiwa ndiyo timu pekee pamoja na Mgambo ambazo hazijapata droo katika ligi ya msimu huu.
Kwenye mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu, Didier Kavumbagu aliyeanza kwa kasi 'amefungwa' spidi gavana kwani mpaka sasa amesaliwa na bao zake nne ambazo zimefikiwa na wachezaji aliokuwa amewaacha nyuma.
Kasi ya washambuliaji wa kizawa inatoa picha kwamba huenda safari hii Kiatu hicho kikatoka mikononi mwa wageni kama alivyoahidi Ali Shomari mwenye mabao mawili anayeichezea Mtibwa.
Ebu angalia msimamo na orodha ya wakali wa mabao mpaka sasa ligi ikienda mapumziko hadi Desemba 27.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                               P   W    D    L    F    A   GD  Pts
01. Mtibwa Sugar    07  04   03  00  10  03  07   15
02. Yanga               07  04   01  02  09  05  04   13
03.  Azam               07  04   01  02  08  04  04   13
04. Coastal Union    07  03   02  02  09  07  02   11
05. Kagera Sugar    07  02   04  01  06  04  02   10
06. JKT Ruvu          07  03   01  03   07  07  00  10
07. Simba               07  01   06  00   07  06  01  09
08. Polisi Moro        07  02   03  02   06  07   -1  09
09. Mgambo JKT     07  03   00  04   04  07   -3  09
10. Stand Utd         07  02   03  02   05   09  -4   09
11. Ruvu Shooting  07  02   01  04   04   07   -3  07
12. Prisons             07  01   03  03   06   07   -1   06
13. Ndanda Fc        07  02   00  05   08   12   -4   06
14. Mbeya City       07   01   02  04   02   06   -4   05

Wafungaji Bora:

4- Didier Kavumbagu(Azam), Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda (Polisi-Moro) Ame Ally (Mtibwa)
3- Ally Shomari (Mtibwa), Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Simon Msuva (Yanga)
2- Shaaban Kisiga (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam), Najim Magulu, Samuel Kamuntu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed (Stand Utd), Ally Nassorm Balimi Busungu (Mgambo)

No comments: