Friday 28 November 2014

Wauza mihadarati Mexiko wawekwa kitimoto

Raisi wa Mexico Enrique Pena Nieto
Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto ametangaza mpango wa utaokasambaratisha mahusiano kati ya mamlaka ya serikali za manispaa ya nchi hiyo na magenge ya wauza mihadarati. Bwana Pena Nieto ambaye pia serikali yake inashutumiwa kufuatia kupotea kwa wanafunzi arobaini 43 katika jimbo la Guerrero amesema Mexico haiwezi kuendelea kama ilivyo sasa.
"Jumatatau ijayo nitatuma mpango wa kubadili katiba katika bunge la Congress kupitisha sheria inayopinga wanajihisisha na uhalifu wa kupanga katika mamlaka ya manispaa. Sheria hii mpya itaanzisha mikakati kwa shirikisho kuanza kazi ya kusimamia shughuli za manispaa au kuziondolea mamlaka kama kuna dalili zinazoonyesha mamlaka hizo zimejihusisha na uhalifu wa kupanga. " Amesema Rais Pena Nieto

No comments: