Thursday 11 December 2014

Baskeli ya tengenezwa kwa dhahabu

Baiskeli ya dhahabu yenye thamani ya shilingi milioni
Ni rahisi sana kwa watu kulalamikia gharama ya kununu baisekli wengi wakitaka bei nafuu. Nyingi ya baiskeli nchini Uingereza huuzwa kwa pauni 1,000 shilingi lakini moja na arobaini pesa za Kenya.
Kwa wengi nchini humo hizo ni pesa nyingi sana.
Gia za baikeli hii zimetengezwa kwa dhahabu
Hata hivyo baikeli mpya iliyotengezwa kwa dhahabu imezinduliwa nchini humo. Bei yake? Pauni laki mbili na hamsini au milioni 36,250,000 pesa za kenya. Bei hii ni ghali hata kuliko bei ya gari jipya la Ferari, kukufahamisha tu.

Baiskeli hio ambayo ilitengezwa na kampuni ambayo hutengeza vitu vya kifahari, Goldgenie imetengezwa kwa dhahabu kutoka kwa mikono na vyuma vyake vyote. Kiwango cha dhahabu iliyotumiwa ni karati 24.
Wataalamu wa kampuni hio ya Goldgenie, wameweka dhahabu katika vyuma vya baiskeli hio vyote , mnyororo na mfumo unaofanya baiskeli kwenda na kubadilisha gia vyote vimewekwa dhahabu.
Mkurugenzi w akampuni iliyotengeza baiskeli hii anasema inaweza kuendeshwa kwa barabara kama baiskeli nyinginezo
Na wakati baiskeli hio inavutia macho, inapowekwa nyuma ya kabati ya glasi na kulindwa na walinzi. Mkrugenzi wa kampuni hio anasema baiskeli hio inaweza kuendeshwa kwenye barabara.
"baiskeli hii sio tu ya kuvutia macho, bali pia ni nzuri ya kuendesha ikiwa mwenye kuiendesha atsatahimili kuangaliwa sana.''
Muundo wa baiskeli hii ni wa hali ya juu,'' aliongeza kusema mkurugenzi huyo.
Kwa sasa haijulikani idadi ya baiskeli hizo zitakazotengezwa, lakini ikiwa utakuwa na bahati sana unweza kupata moja kama hio. Lakini itakubidi ununue kufuli kuifungia baiskeli yako ikiwa hautakuwepo ambako umeiwacha.

No comments: