Tuesday 2 December 2014

Mtanzania matatani kwa madawa ya kulevya huko marekani

Mtanzania aishie Marekani ameshtakiwa kwa kuhusika katika njama ya kimataifa ya kuingiza heroin nchni humo kutoka Tanzania. Mamlaka husika huko Marekani wamemtaja Mtanzania huyo kuwa ni Allen Jordan Baisi (34) na anahusika kwenye mtandao wa kimataifa wa kuingiza madawa ya kulevya Marekani kwa kutumia vifurishi vinavyotumwa kutoka Tanzania kwenda kwa "wateja" mbalimbali Marekani.
Hata hivyo, "wateja" hao walikutwa kuwa ni wasaidizi wake wakuu katika biashara yake haramu ya heroin. Kwa mujibu wa nyaraka za kimahakama, mtandao wake unajumuisha kusafirisha heroin iliyofichwa ndani ya soli za makubadhi (sandals) kwenye vifurushi vilivyokuwa vinatumwa kutoka Tanzania kwenda kwenye anwani za nyumbani zilizoko katika kaunti ya Muskegon.
Kwa mujibu ya wa tovuti ya mlive.com, Allen Jordan Baisi, ambaye anaishi Mount Prospect, Ill, alikamtwa huko Illinois na kushshtakiwa mwezi Octoba mwaka huu kwa kosa la kujihusisha kusambasa karibu gramu 100 za heroin na kosa la money laundering. Kwa mujibu wa nyaraka za kimahakama, Allen Jordan Baisi, ni Mtanzania na alikamatwa kwenye trafiki September 22 mwaka akiwa njia kuelekea uwanja wa ndege kuja Tanzania. Kesi yake itaanza kusikilizwa Januari 6, 2015.
Bw. Baisi anashtakiwa pamoja na watuhumiwa wengine ambao wanajulikana kwa majina na wengine hawajulikani. Waendesha mashtaka wanadai kuwa heroin ilikuwa inafichwa kwenye vifurishi vya nguo ambavyo vilikuwa zinatumwa kwenye anuani za nyumbani zilizopo katika kaunti ya Muskegon na kuwa mtu mwingine ambaye nyaraka za kimahakama zinamtambulisha kama "Individual A” alikuwa anapokea heroin hiyo na kuisambaza eneo hilo. Mtu huyo alikuwa anakusanya malipo kutoka kwa wateja na kuyawasilisha kwa Bw. Baisi huko Illinois ambaye alikuwa anazituma Tanzania na kubakia na nyingine.
Mwaka 2013 na 2014, Bw. Baisi alipokea fedha kama malipo halafu akazituma jiji Dar Es Salaam kama malipo ya alikonunua heroin hiyo. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Homeland Security ya Marekani kwenye simu mbili za Bw. Baisi Ocktoba 7 mwaka huu baada ya kukamatwa, mtuhumiwa aligundulika kuwa kwenye sehemu ya mtandao wa kimataifa wa biashara ya heroin na money laundering kati ya Tanzania na Marekani.
Kwa mujibu wa ripoti ya Homeland Security, wanachama wa mtandao huo wanaishi sehemu mbalimbali duniani zikiwemo Tanzania, India, kaskazini mwa Illinois and magharibi mwa Michigan. Bw. Baisi anadaiwa kusimamia na kufuatilia kwa njia ya kieletroniki jinsi vifurishi hivyo vilivyokuwa vinasafirishwa kutoke Tanzania hadi Muskegon.
Mamlaka husika zilishtukia biashara hiyo ovu Disemba 2013 baada ya kukamata vifurishi viwili (Express Mail parcels) vilivyokuwa vimetumwa kwa wakazi wawili katika eneo la Muskegon. Kila kifurishi kilikuwa na karibu gramu 150 za heroin iliyokuwa imefichwa ndani ya soli za sandals. Uchunguzi ulidumu kwa miezi kadhaa kabla ya kukamata kifurishi cha tatu chenye heroin July 2014 katika uwanja wa John F. Kennedy Airport jijini New York kilichokuwa kinaenda katika anwani iliyopo magharibi mwa Illinois iliyokuwa na uhusiano na Bw, Baisi.
Baisi alikuwa bado anatumikia kifungo cha nje tokea mwaka 2009 baada ya kufungwa kwa kosa la kujihusisha na biashara ya heroin. Agosti 5 mwaka huu, Polisi walimhoji Baisi nyumbani kwake Illinois. Inadaiwa kuwa katika mahojiano hayo, Bw. Baisi alikiri kujihusisha katika mtandao wa biashara ya madawa ya kulevya na money laundering kati ya Tanzania na Marekani.
Baada ya Bw. Baisi kushirikiana na polisi waliokuwa wanafanya uchunguzi, ikiwa ni pamoja na kuwakabidhi simu zake Augosti 25, polisi walipokea taarifa Septemba 19 kuwa angeweza kuondoka Marekani Septemba 22. Maafisa wa Customs waliidhibitishia polisi kuwa Baisi alikuwa amepanga kuondoka na ndege ya Emirates kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa O.Hare kwenda Dar Es Salaam, Tanzania, kinyume na makubaliano ya yeye kutumikia kifungi cha nje.
Baada ya kuambiwa hivyo, polisi walipata warrant na kumkamata Septembe 22 kwenye taa za trafiki maeneo ya Mount Prospect wakati akielekea uwanja wa ndege kurudi Tanzania. Oktoba 30, mahakama iliamua kumweka ndani bila bail kusubiri kesi yake. Jaji alisema Baisi ametenda kosa ambalo adhabu yake ni si chini ya miaka 10 jela na kwamba kuna uwezekano kuwa Baisi angeshindwa kutokea mahakamani au kuhatarisha maisha ya mtu mwingine au jamii kama akiachiliwa.

No comments: