Tuesday 27 January 2015

Chadema yaungana na wananchi kupinga Viongozi wanaowadharau wananchi

Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema mkoani Arusha kimesema kitaendelea kuungana  na wananchi kukemea na kukabiliana na viongozi  wanaowakejeli na kuwakatisha tamaa watanzania wanaotaka kuwekeza kwenye miradi mikubwa ukiwemo wa gesi na mafuta kwani kuendelea kuwafumbia macho ni kuendekeza umaskini.
Akizungumzia mabadiliko hayo katibu wa chama hicho Bw Kalst Lazaro amemtahadharisha Waziri Mh George Simbachawene aliteuliwa kuchukua nafasi ya Prof Muhongo aliyejizulu kuacha kuendelea kuwakatisha watanzania tamaa badala yake awape moyo na kuwasaidia kufikia ndoto zao.
 
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wamesema mtu yeyote anayekatisha wenzake tamaa badala ya kuwapa moyo ni ishara ya kutosha kuwa amepoteza sifa ya kuwa kiongozi na pia uwezo wake wa kuleta mabadiliko ni mdogo kwani hakuna lisilowezekana.

No comments: