Friday 30 January 2015

Diego Costa kuikosa Man city kesho

Diego Costa
Mchezaji wa Chelsea Diego Costa amepigwa marufuku ya mechi tatu kwa kumkanyaga makusudi mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Costa mwenye umri wa miaka 26 atakosa mechi ya wikendi dhidi ya Mancity pamoja na mechi dhidi ya Aston Villa na Everton.
Shtaka hilo ambalo Costa alilikana linatokana na kisa cha mchuano wa kombe la leage Cup raundi ya pili ambapo Chelsea iliibuka kidedea.
Costa aliyesajiliwa kwa kitita cha pauni millioni 32 ana mabao 17 katika mechi 19 za ligi ya Uingereza msimu huu.
Kisa hicho hakikuonekana na maafisa waliosimamia mechi hiyo lakini kilionekana katika kanda ya video.

No comments: