Friday 30 January 2015

Lusinde awapongeza Polisi kwa kumpiga Lipumba

Kulikuwa  na  mvutano  mkali  sana  bungeni  wakati  wabunge  wakijadili  hoja  ya  Lipumba  kupigwa. Hapo  chini  nimekuwekea  michango  ya  Lusinde  na  Sadifa  waliyoitoa  Bungeni:
  Lusinde: Kwani kupigwa Lipumba ndiyo tatizo, wamepigwa viongozi wangapi hapa, Lipumba siyo wa kwanza kupigwa 
Lusinde: Nawapongeza Polisi safari hii kapigwa muhusika mwenyewe, ndiyo nzuri hiyo, siyo wapigwe wengine, kupigwa kazini ndiyo sawa

Lusinde: Bunge linapokwenda mwishoni wabunge wenye hali mbaya majimboni wanakuwa na hamsha hamsha ili wafikiriwe
 
Lusinde: Nawashauri wapiga debe mkiona watu wanaandamana magari hayatembei hampati pesa na nyinyi andamaneni.
  
Sadifa: Mnasema Lipumba kapigwa, hajapigwa hapo, kaguswa tu, huwezi kumlinganisha Lipumba na Kikwete.

No comments: