Saturday 31 January 2015

Waliopanga mbivu za kupindua serikali Gambie waingia matatani

Rais wa Gambia
Waendesha mashtaka nchini Marekani wamewafungulia mashtaka raia wa tatu wa Marekani kwa kuhusika kwenye njama ya mapinduzi nchini Gambia.
Alagie Barrow aliye na uraia wa Marekani na Gambia alifikishwa mahakamani kwenye jimbo la Minnesota akikabiliwa na mashtaka ya kuendesha harakati za kijeshi dhidi ya nchi rafiki.
Taarifa ya mahakama ilisema kuwa bwana Barrow alishukiwa kusaidia kupanga mapinduzi hayo.
Mapinduzi hayo yalifeli wakati walinzi wa rais walipowafyatulia risasi wale waliojaribu kuendesha mapinduzi hayo ambayo baadaye walisafiri kwenda nchini Marekani ambapo walikamatwa.

No comments: