Monday 23 February 2015

Kuchelewa uwanjani kwalobesha Sadio Mane

Sadio Mane anayechezea Southampton

Meneja wa Southampton Ronald Koeman ametoboa siri kuwa jana alilazimika kumwondoa Sadio Mane ambaye ni raia wa Senegal kwenye orodha ya wachezaji watakaonza katika mechi dhidi ya Liverpool kwa kosa la mchezaji huyo kuchelewa kuingia uwanjani.
Koeman amesema ilibidi kumweka mchezaji huyo pembeni na kumpanga mchezaji aliyechukuliwa kwa mkopo kutoka Benifica Philip Jurisichi kuchukua nafasi yake.
Koeman alisisitiza kuwa timu hiyo imejiwekea kanuni ambazo ni lazima kila mtu azifuate .
Katika mechi hiyo Southampton wakiwa nyumbani walipata kichapo cha magoli mawili kwa bila majibu kutoka kwa Liverpool katika mechi ya lidi kuu ya England.
Hata hivyo Koeman amejitetea kwamba pamoja na kipigo hicho cha jana bado ana matumaini kuwa timu yake itamaliza msimu wa ligi hiyo ikiwa katika nafasi nne za juu za msimamo wa ligi.

No comments: