Thursday 30 April 2015

Kocha wa leicester city amtusi mwandishi wa habari baada ya kupokea kichapo toka kwa Chelsea

Kocha wa Leicester City, Nigel Pearson
Meneja wa Leicester City, Nigel Pearson amemshambulia kwa matusi Mwandishi wa habari akimfananisha na ndege aina ya mbuni.
Pearson alifanya kitendo hicho baada ya timu yake kupata kichapo cha 3-1 toka kwa vinara wa ligi Chelsea.
Bosi huyo wa Leicester alimtukana mwandishi Ian Baker aliyemuuliza swali kuhusu madhaifu ya wachezaji wake yaliyosababisha timu kuboronga msimu mzima.
Pearson, hakufurahishwa na namna alivyoulizwa na kuamua kumtukana mwandishi akisema: “Wewe lazima ni punguani sana, sana”.

No comments: