Sunday 3 May 2015

Mayweather ampiga Pacquiao kwa point

Pacquiao na Mayweather
Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa.
Mayweather amshinda Pacquiao
Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.
Pacquiao akimpiga makonde mayweather
Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.
Mayweather ashinda kwa wingi wa pointi
Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.
Mayweather
Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.

No comments: