Wednesday 13 May 2015

Mbatia na Mrema wakutana kanisani wakati wa kumbukumbu za marehemu Baba Stephano Moshi

Mbunge wa kuteuliwa na rais, Jmaes Mbatia akizungumza jambo na mbunge wa jimbo la Vunjo ,Agustino Mrema mara baada ya kukutana kwa mara ya kwanza jimboni humo katika ibada ya kumbukumbu ya askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kanisala la KKKT ,Usharika wa Mamba Kotela ilokofanyika ibada hiyo
Mbunge Mbatia akiingia kanisani humo.
Ujenzi wa taasisi ya saratani ya Bishop Moshi unaofanyika kando ya Usharika huo.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Bishop Moshi wakiwa katika ibada hiyo.
Viongozi mbalimbali wa dini pia walikuwepo.
Mbunge Mrema akiwa ameketi na mbunge mwenzake Mbatia wakifuatilia ibada hiyo.
Askofu mstaafu Dkt Martin Shao akizungumza wakati wa ibada hiyo.
BabaAskofu Dkt Fredrick Shoo akiongoza ibada hiyo ya kumbukumbu ya miaka 29 ya kifo cha aliyekuwa askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini,Stephano Moshi.
Askofu mstaafu Dkt Erasto Kweka akimzungumzia marehemu Baba Askofu Stephano Moshi jinsi alivyo mfahamu.
Baba Askofu Dkt Shoo akitoa hotuba yake .
Ikafika wakati wa kuchangia ujenzi wa taasisi ya saratani ya Bishop Moshi na aliyealikwa mwanzo alikuwa ni Mbunge wa jimbo hilo Dkt  Mrema .
Dkt Mrema akimtizama mkewe Rose Mrema wakati akitoa pesa kwa ajili ya mchango wa harambee ya kuchangia taasisi hiyo ambapo alitoa kiasi cha sh 500,000.
Baadae ikafika zamu ya Mbatia ambaye alipata nafasi ya kuzungumzakido huku akieleza kuwa tayari amekwisha changia kiasi cha Sh Mil 10 kwa ajili ya shule ya sekondari ya Bishop Moshi na pia alitoa kiasi cha sh Mil 2 kwa ajii ya ujenzi wa taasisi hiyo.
Baba Askofu ,Dkt Shoo akimhukuru Mbatia kwa mchango anaoendelea kutoa kwa kanisa.
Baba Askofu Dkt Shoo akizindua rasmi jengo la kuweka kumbukumbu za Askofu wa Kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini Stephano Moshi.
Baba Askofu Dkt Shoo akiingia katika jengo hilo.
Baba Askofu Dkt Shoo akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu.
Askofu mstaafu ,Dkt  Martin Shao akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu.
Baba Askofu,Dkt Shoo akiweka shada la maua katika kaburi la askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini na kufanya maombi katika kaburi hilo.
Mbunge wa kuteuliwa na rais,James Mbatia akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu ya askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaslazini mStephano Moshi .
Mbunge wa kuteuliwa ,James Mbatia akiweka shada la mauakatika kaburi la Askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya kasakzini ,hayati Stephano Moshi.
Mbatia akizungumzajambo na askofu msataafu Dkt Martin Shao mara baadaya kumalizika kwa ibada hiyo/
Maaskofu wastaafu ,Dkt Erasto Kweka na Dkt Martini Shao wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa kuteuliwa James Mbatia mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kumbu kumbu ya asakofo wa kwanza wa KKKT ,Stephano Moshi.

No comments: