Monday 11 May 2015

Ndugu wa Adebayo aomba radhi kwa niaba ya Adebayo

Adebayor

Ndugu ya mshambuliaji wa klabu ya Tottenham Emmanuel Adebayor ameomba msamaha baada ya nyota huyo kumshtumu katika mtandao wa facebook na watu wengine wa familia yake.
Rotimi Adebayor ameiambia shirika la utangazaji la uingereza BBC kwamba anaomba msamaha kwa makosa aliyofanya,na kwamba angependelea nduguye arudi katika familia.
Emmanuel Adebayor ambaye pia anaichezea Togo alisema wiki iliopita kwamba mzigo wa kifedha wa kuisadia familia yake pamoja na ugomvi katika familia yake umemuahiribia kazi yake.
Amesema kuwa anazitaka familia nyingine barani afrika kupata funzo kutoka kwake.

No comments: