Tuesday 12 May 2015

Wakimbizi toka Burundi hatarini kupata magonjwa ya Mlipuko

Wakati shirika la kimataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR likishindwa kuwahamisha maelfu ya waomba hifadhi, hali ya usalama na hofu ya kutokea kwa magonjwa ya mlipuko imewakumba waomba hifadhi kutoka Burundi ambao wapo katika kijiji cha Kagunga wilayani Kigoma, baada ya idadi yao kufikia zaidi ya elfu sitini huku kukiwa hakuna huduma za msingi katika eneo hilo.
 
Wakizungumza katika eneo hilo ambalo linakabiliwa na changamoto kadhaa zinazotishia usalama kama kutokuwepo kwa maji safi na salama, huduma za afya, chakula na mahema, wameomba kuhamishwa kutokana na hali mbaya iliyopo ambapo kwa sasa hawana mahali pa kujificha mvua wala jua huku wakilazimika kutumia maji ya ziwa Tanganyika   kwa matumizi yote.
 
Huku hali ikiwa mbaya katika kijiji hicho ambacho ndio kinapokea idadi kubwa ya waomba hifadhi toka Burundi, ambao tangu April 26 mara tu baada ya chama tawala nchini Burundi kumteua rais Pierre Nkurunziza kugombea tena urais walianza kukimbia kutokana na hofu ya kutokea mapigano baada ya kuwepo maandamano yanayoendelea katika mji mkuu wa Burundi Bujumbura.
 
Shirika la kuhudumia wakimbizi duniani UNHCR ambalo linatumia meli moja Mv Liemba kuwahamishakatika kijiji hicho limeshidwa kutokanana idadi kubwa ya waomba hifadhi wanaoingia kila siku katika kijiji hicho ambacho kipo kandokando ya ziwa Tanganyika.

No comments: