Wednesday 24 June 2015

Liverpool imesajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino

Liverpool imesajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino
Klabu ya Liverpool imemsajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino kutoka klabu ya Hoffenheim kwa kanadarasi ya miaka mitano itakayogharimu pauni millioni 29.
Mkataba huo utaandamana na ukaguzi wa kimatibabu ambao utafanyika baada ya mchezaji huyo kurudi kutoka Chile ambapo amekuwa akiichezea Brazil katika michuano ya Copa America.

Firmino ambaye amefunga mabao 47 katika mechi 151 akiwa katika kilabu ya Hoffenheim atakuwa mchezaji wa pili wa Liverpool aliyeghali mno.
Kilabu hiyo ya Anfield ilimfanya mchezaji Andy Carroll kuwa mchezaji ghali alipojiunga nayo kwa kitita cha pauni milioni 35 kutoka Newcastle mwaka 2011.

No comments: