Monday 27 July 2015

Obama Awasili Ethiopia

Rais Obama akishuka kutoka ndani ya ndege ya Rais
Rais Barack Obama wa Marekani hatimaye amefika nchini Ethiopia katika ziara yake ya pili ya nchi za Afrika.
Ni mara yake ya kwanza tangu aongoze taifa la Marekani akiwa raisi kuhutubia wanachama hamsini na mbili wa umoja wa Afrika katika makao makuu yake yaliyoko Addis ababa.Mazungumzo yao yakiwa yamelenga kutafuta suluhu ya kutokomeza migogoro ya vita za wenyewe kwa wenyewe sudan ya kusini.
Raisi Obama,aliwasili nchini Ethiopia akiwa anatokea mjini Nairobi ambako aliwaambia wakenya kuwa amna kikomo cha kile wanachokihitaji na kusisitiza kwa kutoa angalizo katika athari za ukabila na rushwa. Tamaduni mbaya kama unyanyasaji wa kijinsia,ndoa za kulazimishwa ,tohara kwa watoto wa kike na kutopeleka watoto shuleni.

No comments: