Monday 10 August 2015

Katibu mwenezi wa Chadema achukua fomu kugombea ubunge kupitia ACT-wazalendo.

Aliyelkuwa katibu mwenezi wa chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema katika wilayaya Butiama Bw Richard Choge Magori amekihama chama hicho kisha  kuijunga na chama cha ACT wazalendo kabla ya  kuteuliwa kwa ajili ya kugombea ubunge katika jimbo jipya la Butiama mkoani Mara.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu na mkurugenzi wa wilaya ya Butiama kwa niaba ya tume ya taifa ya uchaguzi ili kumwezesha kugombea ubunge katika jimbo hilo, kada huyo mpya wa chama cha ACT- wazalendo, amesema kuwa ameamua kujiunga na chama hicho na kugombea ubunge katika jimbo hilo baada ya kubaini wanachama
walipendekezwa kugombea ubunge katika jimbo hilo mh Nimrod Mkono wa CCM na Bw Yusuf Kazi wa chadema hawana uwezo wa kutatua matatizo ya wananchi wa jimbo hilo jipya.

No comments: