Tuesday 29 December 2015

Arsenal yapaa kileleni

Washika bunduki wa London, Arsenal wamekaa kileleni mwa ligi ya England kwa pointi 39 baada ya kuichapa Bournemouth kwa mabao 2-0.
Arsenal walipata mabao yao kupita kwa beki Gabriel Paulista aliyefunga bao la kwanza Dakika ya 27 ya mchezo kisha kiungo wa Kijeruman Mesut Ozil, akahitimisha kazi kwa bao la pili alilolifunga katika dakika ya 63.

Nao Mashetani Wekundu wa Man United wakaenda sare ya 0-0 na mabingwa watetezi Chelsea, Everton wakicheza katika dimba lao la Goodson Park wakalala kwa kipigo cha mabao 4-3 dhidi ya Stoke city. Matokeo mengine ni:
Crystal Palace 0 – 0 Swansea Norwich 2 – 0 Aston Villa Watford 1 – 2 Tottenham West Brom 1 – 0 Newcastle West Ham 2 – 1 Southampton

No comments: