Saturday 12 December 2015

Ronaldo atarajia kugombea urais wa shirikisho la kandanda la Brazil

Ronaldo apanga kuwa kiongozi wa CBFRonaldo atarajia kugombea urais wa shirikisho la kandanda la Brazil

Nyota wa zamani wa soka wa Brazil Ronaldo, ametangaza uwezekano wake wa kugombea nafasi ya urais wa shirikisho la kandanda la Brazil CBF.
Ronaldo alitoa tangazo hilo baada ya rais wa CBF Marco Polo del Nero kukabiliwa na kashfa za ufisadi kutoka kwa viongozi wa Marekani.
Naibu wa rais wa CBF Jose Maria Marin pia aliwahi kutangaza kuachia ngazi kutokana na kashfa za ufisadi zilizomuandama mwezi Mei.
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Sao Paulo, Ronaldo alimshutumu Del Nero kwa kutumia mbinu ya kumchagua Antonio Nunes kuziba nafasi ya Marin kwa lengo la kuendeleza ufisadi.

No comments: