Wednesday 6 January 2016

Polisi wakamata silaha kadhaa nchini Kenya

Polisi wakamata silaha kadhaa nchini KenyaSilaha kadhaa zakamatwa kwenye nyumbani moja ya mshukiwa wa ugaidi mjini Mombasa

Maafisa wa polisi nchini Kenya wamekamata silaha kadhaa baada ya kuvamia nyumba moja ya mshukiwa wa ugaidi iliyoko mjini Mombasa.
Silaha hizo zilizokamatwa zilikuwa ni bunduki aina ya G3 na risasi zake 20, bunduki aina ya M4 na risasi zake 7, pamoja na risasi nyingine 318 za ziada.
Wakati huo huo, kompyuta moja na simu 15 za rununu pia zilipatikana kwenye nyumba hiyo.
Silaha na vifaa hivyo vya mawasiliano vinadaiwa kupangwa kutumika katika utekelezaji wa mashambulizi ya kigaidi mjini humo

No comments: