Thursday 31 March 2016

Mahakama yatupilia mbali kesi Uganda


Mahakama ya juu zaidi nchini Uganda imefutilia mbali kesi iliyokuwa ikipinga ushindi wa rais Yoweri Museveni katika uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi uliopita.
Mahakama hiyo ilisema kuwa licha ya kuwepo kwa dosari nyingi za uchaguzi, matokeo ya mwisho hayakuathiriwa.

Kesi hiyo iliwasilishwa na aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo amama mbabazi ambaye alimaliza katika nafasi ya tatu.
Kizza Besigye angali anatumikia kifungo cha nyumbani
Kizza Besigye ambaye alimaliza wa pili amesema hakupata nafasi ya kuwasilisha kesi hiyo mahakamani kwa sababu angali anatumikia kifungo cha nyumbani.
Waangalizi wa kitaifa na kimataifa walishutumu uchaguzi huo ambao ulishindwa na rais Museveni.

No comments: